Tunatoa elimu bora inayolenga kuwafanya wanafunzi kuwa bora kitaaluma pamoja na kujenga ushindani wa kitaaluma nchini.
Shule ipo katika mazingira rafiki ambayo yanamwezesha mwanafunzi kujifunza na kujisomea kwa ufanisi zaidi.
Tunawajenga wanafunzi katika maadili mema, utu, upendo na kuthaminiana.
"EDUCATION & MORALITY"
Karibu Shule ya sekondari ya ST John Paul II.
Lengo letu ni kuwawezesha wanafunzi kupata maarifa ambayo yatawasaidia
kuwa bora katika taaluma kitaifa pamoja na kuwapa elimu itakayowasaidia
kutatua changamoto mbalimbali katika maisha.
Shule ya sekondari ya ST John Paul II imejikita kutoa elimu bora kupitia ufundishaji bora pamoja na mifumo mizuri ya kujifunza na kujifunzia kwa wanafunzi pia, kutengeneza mazingira ya upendo na umoja na kuishi kama familia.
Shule imesajiliwa kwa namba ya usajili S.5107
Masomo
Wanafunzi
Maabara
Walimu
Shule imekuwa ikifanya vizuri kitaaluma katika ngazi ya wilaya, mkoa na taifa na kutoa matokeo mazuri kwa wanafunzi wake katika mitihani ya taifa kama inavyoonekana kwenye jedwali hapo chini:
| MWAKA | I | II | III | IV | 0 |
|---|---|---|---|---|---|
| 2022 | 39 | 6 | 0 | 0 | 0 |
| MWAKA | I | II | III | IV | 0 |
|---|---|---|---|---|---|
| 2022 | 26 | 6 | 0 | 0 | 0 |